MAISHA YENYE FURAHA NA AMANI KATIKA NDOA.
MHUBIRI 9: 7-9
“Enenda zako ule chakula chako kwa FURAHA unywe Mvinyo yako kwa moyo wa KUCHANGAMKA kwa kuwa Mungu amekwisha kukubali kazi zako mavazi yako yawe meupe siku zote na kichwa chako kisikose MARHAMU.
UISHI KWA FURAHA NA MKE UMPENDAYE SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO- ya ubatili ulizopewa chini ya jua…………….
-Nyumba na mali ni URITHI apatao mtu kwa babaye – BALI MKE mwenye BUSARA… MTU- hupewa na Bwana Mith 19:14.
-Kila Mwanamke mwenye Busara hekima hujenga Mith 14:1
-Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima. Mith. 11:16 Mwanamke mwema ni taji ya
Mumewe Mith 12:4.
-Mke mwema kima chake chapita LULU SAFI –chapita utajiri wote wa Marekani na
Japani Mith 31:10.
-MUME wa MKE hujulikana popote kwa ajili ya mke wako Mith 31: 23.
-Nawe umfurahie mke wa ujana wako ni ayala apendaye na paa apendezaye maziwa yake yakutosha siku zoke. Na upendo wake uushangilie daima Mith. 5:18-19.
-‘Na tamaa yako itakuwa kwa mume wako naye (atakuongoza) atakutawala”. Mw. 3:16.
-Ya kwamba kila mwanamume ATAWALE nyumbani mwake Esta 1:22.
-Simpi ruhusa mwanamke KUMTAWALA. MWANAUME ITIM. 2:12 Ef. 5:22.
TAFADHARI: Mith 1:3-5
-Kijana PATA BUSARA itakayokulinda siku zote za maisha yako na UFAHAMU utakaokuifadhi kila siku mafundisho haya katika maisha yako ya ndoa wewe na mkeo yatakuwa:-
i. Wokovu kwako –kukuokoa usifuate njia za waovu.
ii. Yatakuokoa na mambo ya watu wanenao mambo yaliyopotoka-utayajua
yaliyonyooka. Zab.119;105.
iii. Yatakuokoa na watu waziachao njia za Giza.
iv Yatakulinda na watu wanawanafurahia kutenda mabaya.
v. Yatakuhifadhi na watu waliotoka katika njia zao. Watu wakaidi katika mapito yao.
vi. Yatakuokoana Mwanamke Malaya atakayetaka kukupata kwa UBEMBELEZI wa maneno yake.
vii. Yatakuokoa na watu wale waliosahau agano la ndoa zao.
Watu waliosahau Agano la Mungu La Ndoa.
a) Nyumba zao zinaelekea mauti
b) Mapito yao yanaelekea kwa wfu (kuzimu).
KAMA UKIAMBATANA NA WATU WA JINSIA HII NDOA YAKO NAFSI YAKO UZIMA WAKO VYOTE PAMOJA NA WEWE MTAANGAMIA. (MITH 3:1-4).
KIJANA YASHIKE MAFUNDISHO HAYA KWA MOYO WAKO. UYAANDIKE KATIKA KIBAO CHA MOYO WAKO NA HESHIMA
(katika ndoa yako)
MAANA KAMILI YA KUMPA KIJANAMAONYO HAYA:Mith. 21:20.
a)Ni ili kijana / binti apate kuenenda katika njia za watu walio wema.(katika ndoa yako) Mith. 21:20-mwanangu wabaya wakikushawishi wewe usikubali) mith 1:10.
(b) Kuna ndoa za waovu na ndoa za wenye haki. Tunalenga kija na ayashike mapito ya wenye haki.katika ndoa yake.
(a)Maisha ya ndoa yawe na UNYOFU na UKAMILIFU-ili ndoa yenu iweze kudumu hapa ulimwenguni. (ndoa zenye hila zitang’olewa.)
MATUMIZI YA ULIMI KATIKA NDOA YAKO KIJANA - NDOA NYINGI SANA ZIMEFAULU AU KUHARIBIKIWA KWA MATUMIZI MAZURI AU MABAYA YA ULIMI.
HEBU TUANGALIE KATIKA MAANDIKO ULIMI UNA NINI ?
1. Wimbo 4:11 – Bwana Arusi – midomo yako itadondoza asali (maneno matamu) tena chini ya ulimi wako kuna maziwa na asali. NI UAMUZI WAKO KUTOA VITU VILIWE NA BIBI ARUSI WAKO.
2. Bwana Arusi –uzima, afya, njema, amni, mafanikio, baraka, neema, uhai- vipo chini ya ULIMI WAKO.UTUMIE VIZURI ili uiponye ndoa yako na mkeo aule- ulimi wako –apate AFYA NJEMA YA ULIMI) Mith 18:21.
3. KIJANA UTAKULA MATUNDA YA ULIMI WAKO UKINENA JEURI UTAVUNA JEURI –UKINENA UZIMA UTAPATA UZIMA.USITARAJIE KUNENA OVYO-UJIBIWE WEMA, USIMLAANI BIBI ARUSI WAKO USILETE MAUTI KATKA NDOA YAKO KWA ULIMI WAKO. KUMBUKA:Ukinena unapanda ngojea mavuno.
4. KIJANA –UWE MKAMILIFU –ULINDE-
Usijikwae kwa ulimi wako Yak. 3:212 ulimi ni moto.Ulimi ni ule ulimwengu wa uovu. Ulimi utautia au utaitia ndoa yako unajisi –ULIMI: Utawasha moto maumbile yote ya Ndoa yako njema nautayaharibu.
ULIMI:UNACHOCHEWA NA KUZIMU- Ni kiungo chenye msukumo na JEHANAMU.
ULIMI: HUJIVUNA, HUJIINUA, HUJITUKUZA kwa MAJIVUNO makuu mno.
ULIMI: Ni uovu usiotulia - YESU tu anaufunga.
ULIMI: Umejaa sumu iletayo mauti. Bwana Arusi: Panga ni jema ukitumia kwa matumizi mema. Na ULIMI ni mzuri ukiutumia kwa vizuri.
ULIMI: Ni mzuri kwa wale wautumiao vizuri na wanafurahia matunda yake.
ULIMI: Kwa mtu mbaya katika moyo wake anatoa mambo mabaya. Mt. 121:34-35- kwa maneno yako utahesabiwa haki na kwa maneno yako utahukumiwa.
ULIMI:Utayatambulisha yaliyoko katika moyo wako.
ULIMI: Unaweza ukautumia vyema ukatoamaji matamu yenye uzima. Yoh. 4:14.
ILIMI:Unaweza ukaazimu ukatoa maji machungu.
ULIMI: Maneno yake nikama maji ya vilindi kijito kibubujikacho chemchem ya hekima.
ULIMI: Huita mapigo, huita mikosi, huita balaa, huita umaskini.
ILIMI: Utaangukia msiba ukiwa na ulimi mpotofu. Mith 17: 20.
ULIMI: Huchochea magumu mith 15:18, mith 17:14, acheni ugomvi kabla haujafurika.
TUMIA ULIMI WAKO VIZURI : Mith
Usiwe mkorofi- ukamvunja mkeo ulimi wako tu. Uwe na ulimi safi ili NDOA YAKO IWE NA UZIMA – uwepo uzima katika nyumba yako.
FIKIRI UTAKAVYOMJIBU MKEO